Tuesday, June 25, 2013

WAHARIRI/WAANDISHI WAANDAMIZI WAWEKA MAAZIMIO YA KUPAMBANA NA UJANGILI WA TEMBO MJINI IRINGA

JESHI la Polisi mkoani Ruvuma kwa kushirikiana na maofisa Wanyamapori katika Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma limekamata meno ya tembo 18 yenye thamani ya sh milioni 216.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Deusdedit Nsimeki, alisema alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.
Nsimeki alisema kuwa tukio hilo limetokea Juni 20, mwaka huu majira ya saa tisa usiku nje kidogo ya Kijiji cha Majala, Kata ya Nandepo, katika Wilaya ya Tunduru, ambapo askari polisi wakiwa doria waliwaona watu wanne wakisukuma baiskeli zao kuelekea katika kijiji hicho.
Kamanda Nsimeki alisema watu hao walipoona mwanga wa taa za gari la polisi walishtuka na kuzitupa baiskeli zao nne zilizokuwa zimebeba vifurushi na kukimbia.
Alisema askari walipofika eneo zilipotupwa baiskeli hizo na mizigo yake waligundua kuwa ni meno ya tembo 18 yenye uzito wa kilo 84, ambazo zinakadiriwa kuwa na thamani ya sh milioni 216.
Kamanda Nsimeki alisema jeshi hilo mpaka sasa halimshikilii mtu yeyote kuhusu sakata hilo lakini linaendelea na jitihada za kuwatafuta waliozitelekeza baiskeli hizo.
Alisema katika kipindi hiki kifupi polisi wamekamata meno ya tembo kwa wingi na tukio hili ni la tano na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano wa taarifa za siri kwa jeshi hilo.
Aliongeza kusema kuwa mafanikio hayo ya kuwakamata waalifu pamoja na majangili mkoani humo kunatokana na jitihada mbalimbali zinazofanywa na watendaji wa jeshi hilo.
Kamanda Nsimeki alisema vita ya kupambana na wawindaji na wafanyabiashara ya meno ya tembo au rasilimali nyingine za taifa zinahitaji ushirikiano wa kila mwananchi.
Katika hatua nyingine, baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Songea wameiomba Wizara ya Maliasili na Utalii kutoa zawadi kwa wasamaria wema wanaotoa taarifa sahihi za kuwafichua watu wanaojihusisha na biashara ya meno ya tembo.


 MENEJA UHUSIANO WA TANAPA PASCHAEL SHELUTETE AKITOA UFAFANUZI JUU YA SEMINA YA WAHARIRI WA HABARI/WAANDISHI WAANDAMIZI DHIMA IKIWA NI UMUHIMU WA VYOMBO VYA HABARI KATIKA KUPAMBANA NA UJANGILI WA TEMBO,UKUMBI WA SIASA NI KILIMO MJINI IRINGA







BAADHI WA WASHIRIKI WAKIFUATILIA MAELEZO YA UTANGULIZI
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII BALOZI KHAMISI KAGASHEKI KATIKATI,KUSHOTO KWAKE NI JAMES LEMBELI MWENYEKITI WA KAMATI YA ARDHI MALIASILI NA MAZINGIRA,MCHUNGAJI PETER MSIGWA WAZIRI KIVULI NA KULIA KWAKE NI RC IRINGA DK CHRISTINE ISHENGOMA UKUMBI WA SIASA NI KILIMO

No comments:

Post a Comment