Na Salim
Mohammed,Mwananchi
Posted Ijumaa,Decemba20 2013 saa 11:3 AM
Kwa ufupi
Msagati
alisema kuna baadhi hawana kazi jambo linalowafanya kushinda vijiweni na
kupanga kufanya mambo mabaya.
Handeni.Wafugaji nyuki wilayani Handeni
mkoani Tanga, wameitaka Serikali kuwapatia soko la kuuzia asali ili waepuke kutapeliwa
na walanguzi.
Wamesema
kwa kufanya hivyo, watanufaika na zao hilo na kuwaongezea kipato zaidi
wanachoshindwa kukufikia kwa sasa.
Wakizungumza
na waandishi wa habari jana kwa nyakati tofauti, wafugaji hao walisema Serikali
imeisahau sekta hiyo na hivyo kuitaka kuitangaza pamoja na kutoa elimu kwa
wafugaji mjini na vijijini pamoja na kuwapatia soko la uhakika.
Walisema
kwa sasa hawana soko la uhakika la kuuzia asali yao, hivyo kutegemea mteja
mmoja mmoja na walanguzi kutoka nje ya wilaya na mkoa ni jambo linalowanyima
kipato.
“Tumefurahi
leo waandishi wa habari mmekuja eneo letu, hasa hapa sokoni. Tunashindwa
kufahamu soko la uhakika wa bidhaa yetu ya asali, tunaomba mfikishe ujumbe kwa
Serikali ili iweze kutusaidia,” alisema Juma Msagati
Msagati
alisema kuna baadhi hawana kazi jambo linalowafanya kushinda vijiweni na
kupanga kufanya mambo mabaya.
“Tunataka
Serikali ilete wataalamu kutoa elimu kwa vijana ili waweze kushiriki katika
kazi za ufugaji wa nyuki,” alisema Msagati. Akizungumza kwa niaba ya wenzake
Mkazi wa Misima, Khalid Gharib alisema Wilaya ya Handeni ina misitu mikubwa
ambayo imekuwa ikitumiwa na wafugaji wa nyuki, lakini wamekata tamaa baada ya
kukosa soko
No comments:
Post a Comment